MBUNIFU WA KIAFRIKA, MUSTAFA HASSANALI NCHINI BOTSWANA,GABORONE.

Mbunifu wa Mavazi Mustafa Hassanali kutokaTanzania, akiongozana na mmoja wa wanamitindo kuonyesha vazi la ubunifu katika hafla ya Fashion Week nchini Gaborone,Botswana 13 August 2011.

Pichani Juu na Chini ni wanamitindo wakionyesha vazi la ubunifu la Mustafa Hassanali kutoka Tanzania tarehe 13 august-2011 wakati alipofanya onyesho nchini Gaborena Botswana.

Na.MO BLOG TEAM

Mbunifu  Mtanzania Mustafa Hassanali, ameiwakilisha Tanzania katika Maonyesho ya  wiki ya kwanza ya Fashion Botswana, yaliyofahamika  kama  Color in the desert fashion week.

Katika Maonyesho hayo wabunifu mbalimbali wa kimataifa na wenyeji walihudhuria.

Baadhi ya wabunifu wa kiafrika waliohudhulia ni pamoja na  Taibo Bacar (Mozambique), David Tlale,na Thula Sindi kutoka Afrika kusini, Moo Cow (Kenya),  na Joyse Nyasha Chimanye wa  nchini  Zimbabwe.

Kauli mbiu ya Fashion week mwaka huu,ilikua “Kuongeza tija na maendeleo ya fani ya ubunifu wa mavazi na viwanda vya nguo Botswana”

Akizungumzia Maonyesho hayo Mustafa Hassanali alisema “Kutokana na uzoefu wangu,Botswana ni nchi yangu ya kumi na moja kiafrika na ya kumi na tatu kidunia kufanya maonyesho ya ubunifu,Na ninajisikia faraja na kujivunia kuwa mmoja wa waliohudhuria week ya kwanza ya fashion Botswana,na pia kuwa mmoja wa kuendeleza uhusiano mzuri kati ya Tanzania na Botswana kupitia Fashion. “

 
 
 

About the author

More posts by | Visit the site of Admin

 

 

 

Add a comment

required

required

optional