Wazamiaji wanaotafuta watu walionusurika katika ajali ya kuzama kwa meli ya iliyokuwa ikifanya safari za kitalii iliyopinduka ya Costa Concordia nje ya Pwani ya Toscana nchini Italia wamegundua miili ya watu wengine watano.
Wahanga hao wamepatikana baada ya jeshi la majini la Italia kutumia milipuko kutoboa matundu katika eneo la mbele la meli hiyo ili kuweza kuingia katika maeneo ambayo ni vigumu kufikika ndania ya hiiyo.
Idadi ya watu waliofariki sasa inafikia watu 11 huku wengine kiasi ya watu 12 wakiwa bado hawajulikani waliko.








