Baadhi ya viongozi wa chama cha akiba na mikopo cha wafanyakazi wa manispaa ya Singida. Wa kwanza kulia ni mweka hazina wa manispaa ya Singida Deo na anayefuata ni katibu wa SACCOS ya wafanyakazi wa manispaa ya Singida Richard Kattan.
Kulia ni mweka hazina wa SACCOS ya watumishi wa manispaa ya Singida Agnes Mbuva na kushoto ni Mhasibu Joseph Masele.
Baadhi ya wanachama wa SACCOS ya watumishi wa manispaa ya Singida.(Picha zote na Nathaniel Limu).
Na.Nathaniel Limu
Chama cha akiba na mikopo cha watumishi wa halmashauri ya Manispaa ya Singida (SITCOWS) kinaidai ofisi ya mkurugenzi wa Manispaa hiyo zaidi ya shilingi milioni 50.2.
Katibu wa chama hicho Richard Kattani amesema hayo mjini Singida kwenye mkutano mkuu wa chama hicho.
Kattani amesema kuwa fedha hizo ni marejesho ya mikopo ya watumishi mbalimbali wa Manispaa hiyo ambayo Ofisi ya mkurugenzi ilitakiwa kukata kutoka kwenye mishahara yao.
Hata hivyo amesema licha ya kukata fedha hizo kutoka kwa watumishi hao, Ofisi ya mkurugenzi huyo aijaingiza kwenye akaunti ya chama hicho cha akiba na mikopo fedha yoyote katika kipindi cha kuanzia Juni mwaka jana hadi Januari mwaka huu.
Amesema hali hiyo imeathiri utekelezaji wa majukumu ya chama hicho kutokana na baadhi ya wanachama wake kunyimwa mikopo kwa madeni ya nyuma wakati fedha zao zilishakatwa kwenye mishahara yao na Manispaa kutumia kwa shughuli zake.
Mgeni rasmi kwenye mkutano huo Mrajisi msaidizi wa vyama vya akiba na mikopo mkoa wa Singida Andrew Msafiri, amekitaka chama hicho kuchukua hatua za kisheria dhidi ya ofisi ya mkurugenzi ili iweze kulipa deni hilo haraka.










