RASMUSSEN ASEMA NATO ITAENDELEA NA MAPAMBANO.

Katibu Mkuu wa mfungamano wa kijeshi wa NATO Anders Fogh Rasmussen(Pichani) amesisitiza kwamba jumuiya hiyo itaendelea na operesheni za  kijeshi nchini Afghanistan hadi mwaka wa  2014.

Rasmussen ameitoa kauli hiyo mjini Brussels muda mfupi baada ya kuvuma kwa fununu kuwa NATO inapanga kuyaondoa majeshi yake kutoka Afghanistan.

Waziri wa ulinzi wa Ujerumani Thomas de Maiziere na Katibu Mkuu  Rasmussen wamesema kwamba hapatakuwa na mabadiliko katika mipango ya  NATO.

Sababu ya kutokea mkanganyiko ni kauli zilizotolewa na Waziri wa ulinzi wa Marekani Leon Panetta  zilizoashiria kwamba huenda Marekani ikazimaliza operesheni za kijeshi mwaka ujao.

 
 
 

About the author

More posts by | Visit the site of Admin

 

 

 

Add a comment

required

required

optional