MILLARD AYO AFUNGUKA KWA MO BLOG JUU YA AJALI MBAYA ILIYOWAHI KUMTOKEA MAISHANI.

-PIA AMZUNGUMZIA JINSI ALIVYOONDOKA RADIO ONE NA UHUSIANO WAKE NA MKURUGENZI WA ITV/RADIO ONE.

SEHEMU YA KWANZA.

Kama ilivyo kawaida kwa wataalamu wa masuala ya habari na kijamii wa mtandao wa MO BLOG unaotisha kwa sasa, Mhariri Mkuu wa Mtandao huo Lemmy Hipolite na Meneja Mipango Zainul Mzige ‘hamad’ uso kwa uso na mtangazaji maarufu wa Radio na Televisheni hapa nchini Millard Ayo.

MO BLOG: Hebu Millard tufafanulie zaidi tukio hilo la ajali lilikuaje..?

MILLARD AYO:  Yaani sina la kusema ila kama Mungu asingependa mimi nisingekuwepo duniani, lakini kwa sababu alipenda, ndio maana nipo, hata hili kovu katika kichwa upande wa kushoto lipo. Hapa iliingia chuma, unajua mabasi ya zamani yalikuwa na chuma, sasa ile chuma ilikatika wakati basi likijipiga kwenye mawe kama unavyojua kule ni crater.

Kwa kweli ninachokumbuka ni kuwa gari lilipotulia watu walikuwa wakilia na damu zinatiririka na mimi nilikuwa nimebanwa katika hiyo chuma na nilipotolewa sikukumbuka tena nini kiliendelea.

Ilikuwa mbaya sana kwa sababu lile basi lilikuwa likibiringika kama chupa, hivyo watu wanatupwa  madirishani na kisha gari linawalalia ndio mazingira watu walivyopoteza maisha.

OMG…!!!

MO BLOG:  Kitu kingine ambacho MO BLOG ingependa kufahamu ni kuondoka kwako ITV, fununu zinasema kuwa ulikuwa ni mtiti, ni ya kweli haya?

MILLARD AYO: Ningependa watu wakifahamu ni kuwa mimi sina ugomvi na ITV wala sikuondoka kwa ugomvi.

Kwanza kufanya kwangu kazi ITV naamini Mungu alikuwa anaona na alipanga ndio maana hata hivi sasa kuna uwezekano kuwa nafasi nyingine nilizo nazo maishani kwangu nisingezipata, pengine hata ‘Clouds’ wasingeniona na wasingenifuata.

ITV ndio ilimtambulisha Millard Ayo.

ITV niliondoka vizuri ndio maana nitawaheshimu na nitazidi kuwatangaza vizuri popote nitakapokwenda.

Kwa sasa hapa ‘Clouds Radio’ nafanya show yangu ya ‘Amplifaya’ ambayo ina sehemu inayohusisha Blogs, Facebook na Twitter.

Katika kipengele hicho nasoma sana habari zao wanazo zi’tweet’ na nasema nimezitoa ITV.

 Kusoma mahojiano yote Bofya Hapa

 
 
 

About the author

More posts by | Visit the site of Admin

 

 

 

Add a comment

required

required

optional