RAIS KIKWETE AHUDHURIA MAZISHI YA SHEMEJI YAKE MJINI LINDI LEO.

Rais Kikwete akishiriki katika swala ya kumuombea marehemu mjini Lindi leo Julai 30, 2012.

Rais Kikwete akiweka udongo kaburini wakati wa mazishi ya shemeji yake, Marehemu Amani Kinyozi, katika makaburi ya Mitandi mjini Lindi leo Julai 30, 2012.(PICHA NA IKULU).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Jakaya  Mrisho Kikwete, amewasili mjini Lindi leo, Jumatatu,  Julai 30, 2012 kwa ziara ya siku mbili ambako miongoni mwa mambo mengine atafuturisha wananchi na viongozi wa mkoa wa Lindi.

Aidha, rais Kikwete amehudhuria mazishi ya shemeji yake , Marehemu Amani Kinyozi, aliyefariki siku ya Jumamosi jijini  Dar es salaam.

Rais Kikwete, ambaye ameongozana na mke wake Mama Salma Kikwete, alijumuika na mamia ya wakazi wa mji wa Lindi kwenye mazishi hayo, yaliyofanyika katika makaburi ya Mitandi, mjini humo.

Marehemu Amani Kinyozi, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 45, ameacha mke na watoto wawili.

Enzi za uhai wake marehemu alikuwa mtaalamu wa kutengeneza mifuko ya karatasi, na pia  alikuwa akifundisha kinamama wajasiriamali ufundi huo katika juhudi za kuepukana na matumizi ya mifuko ya plastiki, maarufu kama mifuko ya rambo ya kufungia bidhaa.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

30 Julai, 2012

 
 
 

About the author

More posts by | Visit the site of Admin

 

 

 

Add a comment

required

required

optional