Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini wa dini ya Kiislam, katika swala ya Magharibi wakati alipojumuika na waumini hao katika Futari ya pamoja aliyowaandalia na kufuturu nao Migombani Unguja mjini Zanzibar jana Agosti 01, 2012. (Picha na Muhidin Sufiani-OMR).
Wake wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Zakhia Bilal (wa pili kulia) na Mama Asha Bilal (katikati) wakijumuika na waumini wa dini ya Kiislam, wakati wa futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, kwa waumini hao iliyofanyika Migombani Unguja, mjini Zanzibar jana Agosti 01, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya Waumini wa dini ya Kiislam, baada ya kufuturu nao futari ya pamoja aliyowaandalia Migombani Unguja mjini Zanzibar jana, Agosti 01, 2012.














