Na Nathaniel Limu
Katibu wa BAKWATA mkoa wa Singida,Salim Ngaa amewahimiza waislamu mkoani Singida kushiriki sensa ya taifa inayotarajiwa kufanyika nchini kote agosti 26 mwaka huu,kama njia moja wapo ya kuishukuru serikali kwa mema mengi inayoendelea kuwafanyia waislamu.
Ngaa ametoa wito huo (19/8/2012) wakati akizungumza kwenye sala ya Eid Eliftiri iliyofanyika kwenye uwanja wa michezo wa namfua mjini hapa.
Alisema lengo la serikali kuhesabu watu wake ni kutaka kujua idadi yao ili iwe rahisi kupanga mipango ya uhakika ya kuwaletea maendeleo pamoja na kutoa huduma zitakazokidhi mahitaji ya sehemu husika.
“Ndugu zangu waislamu tusidanganyike kwa lolote lile kuhusu zoezi hili la sensa ya mwaka huu.Tujitokeza wote kabisa na tutoe ushirikiano wa kutosha ili lengo la serikali liweze kufikiwa”,alisema Ngaa.












